Fao la Uzazi

Vigezo vya kujiunga:

  • Mwanachama lazima awe mwanamke mwenye umri wa zaidi ya miaka 18
  • Hutolewa kwa mwanachama mwanamke aliyejifungua mtoto/watoto kila baada ya miaka 3
  • Mwanachama awe amechangia kwa kipindi cha mwaka 1 (miezi 12) mfululizo kabla ya kujifungua
  • Mwanachama awe amechangia kwa kipindi kisichopungua miaka 2 (miezi 24)

Mpango wa malipo:

  • Mwanachama atalipwa kiasi cha Tsh 1,000,000 mara baada ya kujifungua salama
  • Malipo haya yatalipwa hadi mara 4 kila baada ya miaka 3 mara tu mama anapojifungua.
  • Inapotokea mtoto amepoteza maisha ndani ya miezi 12 tokea kuzaliwa kwake, mwanachama ataweza kupata mafao yake bila ya kusubiri hadi miaka 3 ipite.

Fomu zinazohitajika:

  • Fomu ya madai ya PPF iliyojazwa kwa usahihi
  • Barua iliyothibithishwa na mwajiri wako kutoka kwa hospitali ambayo mwanachama anapata huduma za cliniki
  • Nakala ya cheti kilichothibishwa cha kuzaliwa kwa mtoto (yaani Tangazo la kuzaliwa kwa mtoto)